|
|
|||
Imefahamika kuwa wakati ajali hiyo inatokea, watu 528 walikuwa wakifanya kazi chini ya ardhi, na watu 139 miongoni mwao walikumbwa na ajali hiyo. Kati ya hao, watu 31 wameokolewa.
Uchunguzi wa ajali hiyo umeanza, na matokeo ya mwanzo ya uchunguzi yanaonesha kuwa, chanzo chake ni ulimbizaji wa gesi nyingi kupita kiasi kwenye mgodi huo na kupelekea kulipuka.
Rais Hu Jintao wa China na waziri mkuu Wen Jiabao wamemtaka naibu waziri mkuu Bw. Zhang Dejiang aende mahali ilipotokea ajali na kuongoza kazi ya uokoaji.
| © China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |