|
|
|||
Mwenyekiti wa shirika la nishati ya atomiki la Iran Bw. Ali Akbar Salehi tarehe 9 alitangaza kuwa, siku hiyo Iran imeanza kusafisha uranium nzito yenye asilimia 20 ya nyuklia huko Natanz.
Bw. Salehi alisema wakaguzi wa kimataifa watafanya ukaguzi kwenye sehemu ya kusafisha uranium nzito.
Msemaji wa shirika hilo Bw. Ramin Mehmanparast alisema kusafisha uranium nzito yenye asilimia 20 ya nyuklia hakuendi kinyume na lengo la matumizi ya amani ya nishati ya nyuklia, na hakumaanishi kuwa mazungumzo kuhusu nishati ya nyuklia hayawezekani kufanyika. Kama pande husika zitazingatia masharti yaliyotolewa na Iran, mpango wa kusafirisha uranium nzito katika nchi za nje bado unaweza kutekelezwa.
| © China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |