Mkutano wa kwanza wa kamati kuu ya 18 ya Chama cha Kikomunisti cha China umefanyika leo hapa Beijing. Kwenye mkutano huo Bw. Xi Jinping amechaguliwa kuwa katibu mkuu wa kamati mpya ya chama hicho, na Xi Jinping, Li Keqiang, Zhang Dejiang, Yu Zhengsheng, Liu Yunshan, Wang Qishan na Zhang Gaoli wamechanguliwa kuwa wajumbe wa kudumu wa ofisi ya siasa ya kamati kuu ya Chama cha kikomunisti cha China. Mkutano huo pia umeamua Xi Jinping kuwa mwenyekiti wa kamati ya kijeshi ya kamati kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |