Marekani jana iliadhimisha mwaka mmoja tangu utokee mlipuko wa Boston, ili kukumbuka watu waliouawa katika mlipuko huo. Rais Barack Obama wa Marekani alitoa taarifa akikumbushia kuhusu watu wanne waliouawa katika mlipuko huo na mchakato wa kuwasaka watuhumiwa, na kutoa salamu za pole kwa majeruhi. Milipuko miwili ya mabomu ilitokea Aprili 15 mwaka jana katika mashindano ya Marathon huko Boston, na kusababisha vifo vya watu watatu na wengine zaidi ya 260 kujeruhiwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |