Waziri mkuu wa China Bw. Li Keqiang leo amekutana na waziri mkuu wa Madagascar Bw. Kolo Roger ambaye yuko ziarani hapa China kuhudhuria sherehe ya kufungwa kwa Michezo ya pili ya Olimpiki ya Vijana.
Bw. Li Keqiang amesema China inapenda kushirikiana na Madagascar kuimarisha uaminifu, kuhimiza ushirikiano wa kunufaishana katika sekta za nishati, kilimo, mifugo na uvuvi, mafunzo ya nguvukazi na kupunguza umaskini, na kuinua uhusiano na ushirikiano kati ya nchi hizo mbili kwenye ngazi mpya.
Kwa upande wa Bw. Kolo Roger, amesema Madagascar inatarajia kuimarisha mawasiliano ya kirafiki na ushirikiano wa kunufaishana katika sekta mbalimbali kati yake na China.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |