Waziri wa afya wa Nigeria Bw Onyebuchi Chukwu amesema hadi sasa jumla ya matukio matatu ya maambukizi ya virusi vya Ebola yameripotiwa katika jimbo la Port Harcourt. Akizungumza na waandishi wa habari, Bw Chukwu amesema idadi hiyo imefikiwa baada ya vipimo vya wiki iliyopita kuonyesha kuwa mwanamke mmoja na wafanyakazi wawili hospitali wameambukizwa virusi vya Ebola. Daktari mmoja aliyekuwa akiwatibu wagonjwa hao alifariki ndani ya wiki mbili baada ya kuugua ugonjwa huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |