• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Bw Ban Ki-moon ashtushwa na uamuzi wa Israel kutwaa eneo la ardhi ukingo wa magharibi

    (GMT+08:00) 2014-09-02 11:19:56

    Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw Ban Ki-moon ameeleza kushtushwa na Israel jana kutangaza kuwa eneo la Bethlehem kwenye ukingo wa magharibi lenye hekta 400 ni sehemu ya taifa lake. Amesema kujitwalia eneo kubwa la ardhi kama hilo kunaweza kuifanya Israel kujenga makazi mengi zaidi, jambo ambalo ni haramu chini ya sheria ya kimataifa na kwenda kinyume na juhudi za kutafuta suluhisho la kuwepo kwa nchi mbili za Palestina na Israel.

    Bw. Ban pia ameitaka Israel kutii wito wa jumuiya ya kimataifa wa kuacha shughuli za kujenga makazi na kufuata ahadi yake chini ya sheria ya kimataifa. Serikali ya Israel imesema eneo hilo halijatangazwa kumilikiwa na wapalestina, na kuongeza kuwa kuna kipindi cha siku 45 cha kufungua pingamizi dhidi ya uamuzi huo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako