Hafla ya kukabidhi mradi wa ujenzi wa kituo cha mafunzo kwa wanawake nchini Chad uliofanywa kwa msaada wa serikali ya China imefanyika jana mchana katika mji mkuu wa Chad, N'Djamena.
Waziri wa afya ya umma, shughuli za kijamii na mshikamano wa taifa wa Chad amesema, mradi huo ukiwa ni wa kwanza kwa ajili ya wanawake tangu Chad ipate uhuru miaka 50 iliyopita, una umuhimu mkubwa wa kihistoria. Ameishukuru serikali ya China kwa juhudi zake katika kuhimiza maendeleo ya wanawake nchini Chad, na pia anatumai kuwa nchi hizo mbili zitaweza kuimarisha zaidi ushirikiano kwenye sekta ya afya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |