Uchaguzi mkuu wa 11 wa Bostwana umefanyika leo. Upigaji kura umeanza saa 12 na nusu asubuhi na umeendelea kwa utulivu.
Wapiga kura zaidi laki 8.2 kati ya watu milioni 2 wa nchi hiyo watapiga kura katika vituo 57 vilivyowekwa sehemu mbalimbali nchini humo.
Rais wa zamani wa Malawi Bi. Joyce Banda ambaye ameongoza ujumbe wa waangalizi wa Umoja wa Afrika ameeleza kuridhika kwake na maendeleo mazuri ya uchaguzi huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |