Tume ya uchaguzi ya Botswana imetangaza matokeo ya uchaguzi wa ijumaa wa serikali za mitaa yanayoonyesha chama tawala cha Botswana BDP kikiongoza kwa kupata viti vingi. Msemaji wa tume hiyo Osupile Maroba amesema jumla ya kura elfu 160,870 tayari zimehesabiwa ambapo chama cha BDP kinaongoza kwa kupata jumla ya kura elfu 76,214. Awali Maroba alisema walitarajia kukamilisha shughuli ya kuhesabu kura leo adhuhuri.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |