Takriban watu 132 wameuawa na wengine 245 kujeruhiwa baada ya wapiganaji la kundi la Taliban waliovalia sare za kijeshi kufanya mashambulizi leo saa 4 asubuhi kwa saa za huko, katika shule ya umma inayoendeshwa na jeshi huko Peshawar katika jimbo la Khyber Pakhtunkhwa, Pakistan.
Vyombo vya habari vya huko vimesema idadi isiyojulikana ya wanafunzi na walimu wanashikiliwa mateka, na walinzi wa usalama wanapambana na wapiganaji hao na kuwaua wapiganaji watatu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |