Idadi ya watu waliofariki kutokana na mafuriko kaskazini na maeneo ya kati ya Msumbiji imefikia 117, hayo ni kwa mujibu wa idara ya kushughulikia majanga nchini humo. Idara hiyo imesema hadi Januari 25 zaidi ya watu laki mbili walikuwa wameathirika kwenye maeneo hayo huku madarasa 1, 400 yakiharibiwa na masomo ya zaidi ya wanafunzi elfu 78. Serikali za mitaa sasa zinagawa viwanja kwa wahanga ili kuwawezesha kujenga makazi mapya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |