Maonesho ya picha za Asia yaliyoandaliwa na Redio China Kimataifa CRI, Manispaa ya mji wa Sanya, na shirika la utangazaji la Sangya yamefanyika mjini Sanya, mkoani Hainan ikiwa moja ya shughuli za baraza la Boao la Asia linaloendelea mkoani humo, kusini mwa China.
Maonesho hayo yanalenga kuonesha maendeleo mapya yaliyopatikana katika mwaka mmoja uliopita barani Asia.
Mkuu wa CRI Wang Gengnian amesema maendeleo ya binadamu yanatokana na mawasiliano na maingiliano ya staarabu tofauti, na ikiwa chombo cha habari, CRI itaendelea kuimarisha ushirikiano na wenzake kutoka nchi zilizoko kwenye ukanda wa kiuchumi wa njia ya hariri na njia hariri baharini ya karne 21.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |