Rais Xi Jinping wa China atoa hotuba kwenye maadhimisho ya miaka 60 ya mkutano wa baraza la Asia na Afrika Viongozi wa nchi za Asia na Afrika jana walikusanyika Jakarta Indonesia kwenye mkutano wa kuadhimisha miaka 60 tangu kufunguliwa kwa mkutano wa baraza la Asia na Afrika, yaani mkutano wa Bandung. Rais Xi Jinping wa China alitoa hotuba kwenye mkutano huo, na kueleza sura mpya kuhusu jinsi nchi zinazoendelea zinavyoweza kushikamana na kushirikiana ili kufanya kazi kubwa zaidi na kuhimiza maendeleo yenye uwiano duniani katika zama mpya. Pia ameahidi kuwa China daima itakuwa rafiki na mwenzi wa dhati wa nchi zinazoendelea.