Tarehe 22 Aprili ilikuwa ni siku ya sayari ya dunia, siku maalumu iliyopangwa na Umoja wa Mataifa kuwakumbusha watu kuwa na mwamko wa kuwa na mienendo inayolinda dunia yetu. Tunafahamu kuwa dunia yetu ina maliasili zenye ukomo. Matumizi mabaya ya maliasili zinazotumiwa na wengi, kama vile maji, ardhi, mimea yanaweza kuwa na athari mbaya kwa jamii, sio tu kiuchumi bali pia hata kiafya. Kwenye maeneo yenye watu wengi au nchi zenye watu wengi kama China, kunakuwa na shinikizo kubwa kwenye matumizi ya maliasili kiasi kwamba kama hakuna usimamizi wa kutosha kunaweza kuwa na madhara makubwa kwa jamii nzima. Kipindi hiki tunaangalia baadhi ya mambo yanayofanywa na wachina katika ulinzi wa mazingira ya asili ya dunia.
20150423 China Machoni Mwetu
|
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |