Tangazo hilo lisilotegemewa lilitolewa na mwendesha mashitaka wa mji huo Marilyn Mosby likisema kijana huyo mweusi Freddie Gray alikuwa na majeraha mabaya kwenye shingo kutokana na kuwekwa pingu mikononi na miguuni ndani ya kituo cha polisi cha Baltimore.
Tangazo hilo limewapa moyo watu mjini humo ambao wanaendelea kuandamana, wakiwa na tabasamu nyusoni kinyume na hapo nyuma.
Hata hivyo, amri ya kutoruhusu kutembea usiku iliotolewa mjini humo tangu jumatatu iliyopita bado inaendelea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |