Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry amesema, Iran na nchi zenye nguvu duniani zinalenga kumaliza duru ya mwisho ya mazungumzo ya nyuklia katika muda uliopangwa na pande zote.
Akiongea na waandishi wa habari baada ya jana mchana kukutana na mwenzake wa Iran Bw. Mohammad Javad Zarif, Bw. Kerry amesema "sasa ni wakati wa kuangalia kama wataweza kufikia makubaliano au la" baada ya wajumbe wa ngazi wa juu wa nchi mbalimbali jana kurudi tena mjini Vienna kwa ajili ya mazungumzo.
Hata hivyo, licha ya maendeleo halisi yaliyopatikana katika siku zilizopita, Bw. Kerry amesema bado hawajakubaliana juu ya masuala kadhaa magumu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |