Sekta binafsi nchini Kenya na Rwanda zimetangaza kuanza ushirikiano wa kibiashara ili waweze kukuza biashara kati ya mataifa hayo mawili ya Afrika Mashariki.
Sasa wawakilishi wa kibiashara katika mataifa hayo hivi karibuni wanatarajiwa kutia saini makubaliano ya kufanya hiyo.
Makubaliano hayo yakitiwa saini basi yatawezesha mataifa hayo kushirikiana zaidi katika kuendesha biashara katika sekta binafsi na kukuza uchumi wa mataifa hayo pakubwa.
Mataifa ya Afrika Mashariki yamekuwa yakishirikiana katika mambo ya kiuchumi na ushirikiano huo kati ya Kenya na Rwanda huenda ukachochea biashara zaidi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |