Wizara ya fedha ya Kenya imeidhinisha kandarasi ya miaka mitatu ya usambazaji wa mbolea kwa gharama ya shilingi bilioni 6.
Kaimu waziri wa kilimo Adan Mohammed pamoja na katibu wake Sicily Kariuki wamesema wizara hiyo pia imeona ni rahisi kwa Bodi ya nafaka ya Kenya kuchukua bima ya mbolea hizo wakati zinaposafirishwa nchini Kenya. Bi Kariuki amesema hatua hiyo itaifanya serikali ya Kenya kuokoa jumla ya shilingi milioni 200.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |