v Uzinduzi wa Wiki ya Zhengzhou wafanyika Nairobi
Ujumbe kutoka mji wa Zhengzhou nchini China umeandaa maonyesho ya wiki moja ya matangazo ya redio na maonyesho ya picha za mji huo mjini Nairobi.
Maonyesho hayo ya wiki moja yalizinduliwa jana jioni katika hoteli ya Safari Park kwa ushirikiano wa serikali ya mji wa Zhengzhou,ubalozi wa China nchini Kenya na Idhaa ya Kiswahili ya Redio China Kimataifa,kwa ajili ya kuwajulisha wakenya kuhusu historia na utamaduni wa mji wa Zhengzhou,ambao ndio chimbuko la Kungfu ya Shaolin.
|