Msemaji wa Umoja wa Mataifa Bw. Stephane Dujarric amesema, hakuna maambukizi mapya ya Ebola kwa wiki nzima iliyopita, ambayo ni mara ya kwanza baada ya mwezi Machi mwaka 2014 kutokuwa na maambukizi mapya kwa wiki nzima.
Shirika la afya duniani WHO limethibitisha kwenye ripoti yake mpya kuwa hakuna maambukizi mapya ya Ebola katika wiki iliyopita iliyoisha tarehe 4 Oktoba.
Ugonjwa wa Ebola ulilipuka katika nchi za magharibi mwa Afrika mwaka jana, Liberia, Sierra Leone na Guinea ziliathiriwa zaidi na ugonjwa huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |