Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limeanza mchujo wa siku tatu wa wagombea wanane wa nafasi ya katibu mkuu wa Umoja huo akiwemo Igor Luksic kutoka Montenegro akiwa wa kwanza.
Bw Luksic alijibu maswali ya wawakilishi wa Baraza Kuu kuhusiana na mada za udhalilishaji wa kijinsia uliofanywa na walinzi amani wa Umoja wa Mataifa na utekelezaji wa maendeleo endelevu.
Alifuatiwa na katibu mkuu wa shirika la utamaduni la Umoja wa Mataifa la UNESCO Bibi Irina Bokova na aliyekuwa kamishna mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi Antonio Guterres.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |