Messi ambaye ni mshambulizi wa klabu bingwa ya Barcelona, anakabiliwa na mashtaka ya udanganyifu na kukwepa kulipa kodi ya takriban dola milioni 4.5 kati ya mwaka wa 2007 na 2009.
Messi na babake Jorge, ambaye ndiye anayesimamia mali yake wanadaiwa kuficha mamilioni ya pesa katika visiwa visivyotoza kodi vya Belize na Uruguay.
Aidha wawili hao wanadaiwa kudanganya maafisa wa kukusanya kodi walipoulizwa awali katika uchunguzi huo.
Mamlaka ya ushuru ya Uhispania inadai kuwa walitumia visiwa hivyo kuficha malipo ya haki miliki ya sura ya mshambulizi huyo matata na upande wa mashtaka unataka wahukumiwe kifungo gerezani mbali na kutozwa faini kubwa ili iwe mfano kwa wengine wenye nia kama yao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |