Rais wa Burundi awapa waasi makataa ya wiki mbili kujisalimisha.
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amewapatia waasi makataa ya wiki mbili kujisalimisha akisema iwapo hawatasalimu amri atakabiliana nao kwa nguvu.
Rais Nkurunziza alitoa matamshi hayo wakati wa ziara yake katika mji wa Mugamba kilomita 80 kusini mwa mji wa Bujumbura ambao umetajwa kuwa na makundi mengi ya waasi.
Ameonya kuwa vikosi vya usalama vitatumia mbinu kama ]zilizoangamiza maandamano dhidi ya serikali mwaka 2010 ambayo mashirika ya kibinaadamu yanasema yalihusisha unyanyasaji mkubwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |