Walioshambulia ndege ya Somalia wahukumiwa maisha
Mahakama ya kijeshi ya Somalia imewahukumu watu wawili kifungo cha maisha wiki hii kutokana na makosa ya kupanga shambulizi la mabomu kwenye ndege hii ya Somalia mwezi Februari.
Mlipuko ulitokea dakika 15 baada ya ndege aina ya A321 ya shirika la ndege la Daallo kuruka, na kutoboa shimbo kando ya ndege hiyo. Rubani alifanikiwa kurudi na kutua kwenye uwanja wa ndege wa Mogadishu. Abiria mmoja anayedhaniwa kuwa mshambulizi aliuawa na wengine waili walijeruhiwa. Kundi la Al-Shabaab lilitangaza kuhusika na tukio hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |