Jeshi la Sudan latwaa tena eneo la kimkakati kwenye mkoa wa Blue Nile
Jeshi la Sudan wiki hii limetwaa tena eneo la kimkakati kwenye mkoa wa Blue Nile, baada ya kupambana vikali na wapiganaji wa tawi la kaskazini la kundi la waasi la SPLM.
Mkuu wa mkoa wa Blue Nile Bw. Hussein Yassin amesema jeshi la Sudan limepanga kulikomboa eneo la Jebel Kalgo kutoka kwa wapiganaji wa tawi la kaskazini la kundi la SPLM.
Kituo hicho kilinukuu habari kutoka jeshi la Sudan, kikisema kuwa jeshi hilo lilipambana vikali na waasi hao kwenye barabara za eneo la Jebel Kalgo, 30 kilomita kusini mwa Damazin, mji mkuu wa mkoa wa Blue Nile.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |