Kampuni kubwa zaidi ya uundaji wa vifaa vya elektoniki ya China Suning, itanunua asilimia 70 ya umiliki wa klabu ya soka ya Italia, Inter Milan.
Suning italipa dola milioni 360, ilihali tajiri mkubwa nchini Indonesia Erick Thohir atasalia na asilimia zake 30.
Mwenyekiti wa Suning, Zhang Jindong ameutaja ununuzi huo kama hatua kubwa kwa soka nchini China.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |