Maria Sharapova ambaye ni mcheza tennis maarufu duniani ameingia kwenye vichwa vya habari baada ya kuripotiwa kufungiwa kucheza Tennis kwa muda wa miaka miwili na Shirikisho la Tennis la kimataifa duniani (ITF), baada ya vipimo kuthibitisha kuwa anatumia dawa za kuongeza nguvu aina ya Meldonium kwa muda mrefu. Shirikisho hilo limetangaza rasmi Jana kuwa mrembo huyo hatoruhusiwa kucheza tennis kwani amekiuka sheria za michezo, ingawa imetangazwa rasmi kufungiwa kwake, Maria Sharapova anasema yeye amekuwa akitumia dawa hizo kwa matibabu ya moyo tangu mwaka 2006.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |