Mwendesha langalanga Nico Rosberg ametwaa ushindi wa mbio za kwanza za Baku akimuonyesha kivumbi mwezake wa timu ya Mercedes Lewis Hamilton.
Rosberg kutoka Ujerumani hakuwa na kibarua kigumu kutwaa ushindi huo wa Baku kwani kwenye nafasi ya pili alikuwa ni Sebastian Vettel akiendasha Ferrari,.
Hamilton aliridhika na nafasi ya tano baada ya kukumbwa na matatizo ya mara kwa mara kwenye mbio hizo za mizunguko 51.
Hata hivyo Hamilton na Kimi Raikkonen amabye alikuwa kwenye nafasi ya nne wamekabiliwa na tatizo la sheria mpya ya 2016 ambayo inakataza maderefa kupokea taarifa yoyte kupitia kwa njia ya redio wakati wakiwa mbioni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |