Watu zaidi ya 16 wameuawa akiwemo waziri wa mambo ya mazingira wa Somalia na wengine wengi wamejeruhiwa katika milipuko miwili ya mabomu yaliyotegwa ndani ya magari iliyotokea jana alasiri kwenye hoteli moja katika mji mkuu wa nchi hiyo, Mogadishu.
Ofisa wa polisi nchini Somalia Mohamed Nor aliyeshuhudia shambulizi hilo amesema, wengi wa waliouawa ni raia wa kawaida waliokuwa katika hoteli ya Nasa-Hablod wakati milipuko ilipotokea.
Kundi la Al-Shabaab limetangaza kuhusika na shambulizi hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |