Matokeo ya hesabu ya kura zilizopigwa kwenye uchaguzi wa bunge la Hispania yanaonesha kuwa, chama tawala cha nchi hiyo kimeshindwa kupata kura za kutosha kukiwezesha kuongoza peke yake. Hii inaamaanisha kuwa ingawa chama hicho Partido Popular kimepata kura nyingi zaidi, kinatakiwa kutawala kwa kushirikiana na vyama vingine, kama ilivyokuwa baada ya uchaguzi wa bunge wa Desemba mwaka jana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |