Mfalme Mohammed VI wa Morocco amezindua daraja lililojengwa na kampuni ya China ambalo ni kubwa zaidi la kuning'inia barani Afrika.
Mfalme huyo amewashukuru wafanyakazi wa China na kusema ujenzi huo umetimiza ndoto ya watu wa Morocco ya miaka 30 iliyopita.
Daraja hilo lenye urefu wa mita 952 na upana wa mita 30.4 linaunganisha mji mkuu wa Morocco Rabat na mji wa kaskazini magharibi Sale, na ni daraja la kwanza la kisasa la aina hiyo barani Afrika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |