Kwa mujibu wa Ratiba ya Ligi Kuu iliyotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) michuano hiyo itaanza Agosti 20 kwa mechi saba kuchezwa kwenye viwanja tofauti, ikitanguliwa na mchezo wa Ngao ya Jamii kati ya Azam na Yanga Agosti 17, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi za ufunguzi za Ligi Kuu Agosti 20, Simba SC watacheza na Ndanda FC Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, huku Azam wakiikaribisha African Lyon Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |