Mgombea wa chama cha upinzani cha Republican nchini Marekani Donald Trump amehitimisha mkutano mkuu wa siku 4 wa chama chake mjini Cleveland kwa kuwahutubia maelfu ya wafuasi wa chama hicho
Donald Trump kwenye hotuba yake ameahidi kumaliza uhalifu na ghasia nchini Marekani iwapo atachaguliwa kuwa rais kwenye uchaguzi mkuu mwezi Novemba na kwamba hakuwezi kuwa na ufanisi bila kuwepo utawala wa sheria.
Aidha, ameahidi kuchukua hatua kali kukabiliana na wahamiaji haramu na akaonga kuwa kwa sasa wahamiaji wanaruhusiwa kuingia na kuishi katika jamii za Marekani bila kuzingatia usalama wa umma.
Bw Trump amejieleza kama mkombozi na sauti ya wanyonge na watu waliosahaulika nchini Marekani, na akajionyesha kama mtu mwenye sifa tofauti na mpinzani wake wa chama cha Democratic Hillary Clinton ambaye sana amemuonesha kama mtu mfisadi na asiyewajibika.
Salva Kiir, ametoa wito kwa Riek Machar kurejea Juba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |