Tamasha la siku nne la vijana wa China na Afrika kwa mwaka 2016 limefungwa mjini Guangzhou, ambapo vijana wapatao 200 kutoka nchi za Afrika na wenzao wa China wameshiriki katika shughuli mbalimbali zinazolenga kuongeza maelewano kati yao.
Kijana Leonald Ngeny kutoka Kenya amemwambia mwandishi wetu wa habari kuwa hii ni ziara yake ya kwanza nchini China, na amevutiwa sana na miji mbalimbali aliyotembelea.Amesema baada ya kurudi Kenya, atawaambia marafiki zake kuwa China ni tofauti na walivyosikia awali, na atawaelezea mambo aliyojionea katika ziara yake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |