Timu ya Yanga ya Dar es Salaam imeaga mashindano ya kombe la shirikisho kwa kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa TP Mazembe ya DRC.
Mechi hiyo ya marudiano ya Kundi A ambayo imepigwa mjini Lubumbashi nchini DRC, ilikuwa na umuhimu wa kuweka heshima kwa Yanga kwa kumaliza ikiwa na point 7 jambo ambalo limeshindikana.
Katika mchezo mwingine, Medeama ya Ghana imekubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa MO Bejaia nchini Algeria, na kufanya msimamo wa kundi A ubadilike, hali iliyopelekea Medeama kuungana na Yanga kufungasha virago.
Msimamo wa kundi hilo unaonesha kuwa TP Mazembe ndiyo vinara wakiwa na point 13 wakifuatiwa na MO Bejaia yenye point 8 ikilingana na Medema yenye point 8 pia, huku wakilingana tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa, na Yanga inakamata mkia ikiwa na point 4.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |