Klabu ya Arsenal imemtoa kwa mkopo mchezaji wao kiungo wa kati wa Uingereza Jack Wilshere na kwenda klabu ya Bournemouth, ili kupata fursa ya kujumuika katika kikosi cha kwanza cha timu ya taifa.
Wilshere mwenye umri wa miaka 24, ambaye amekuwa majeruhi kutokana na jeraha la mguu aliichezea Arsenal mara tatu pekee msimu uliopita baada ya kupata jeraha hilo. Na pia aliichezea Uingereza mara sita pekee msimu ulioipita, ikiwemo mechi tatu katika mashindano ya Euro2016, lakini hakuchaguliwa katika kikosi cha kwanza cha mkufunzi Sam Allardyce wiki hii. Arsenal kwasasa imefanya usajili wa mchezaji wa Switzerland Granit Xhaka kwa pauni milioni 35 katika msimu huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |