Mkutano wa kilele wa Kundi la G20 umefunguliwa leo alasiri katika Kituo cha Maonyesho ya Kimataifa mjini Hangzhou, China. Rais Xi Jinping wa China ameendesha na kuhutubia ufunguzi wa mkutano huo.
Katika mkutano huo wa siku mbili wenye kaulimbiu ya "kujenga uchumi wa dunia unaoungana wenye uvumbuzi, uhai, na ushirikishi", viongozi wa nchi wanachama wa Kundi la G20, nchi wageni na mashirika ya kimataifa watajadiliana kuhusu masuala makuu ya kiuchumi, yakiwemo "kuimarisha uratibu wa kisera, kufanya uvumbuzi kwa njia ya kukuza uchumi", "usimamizi wenye ufanisi wa kiuchumi na kifedha duniani", "biashara na uwekezaji wa kimataifa" na "maendeleo ya kiuchumi yenye ushirikishi na muungano".
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |