Valencia CF ipo mkiani mwa msimamo wa ligi ya Hispania La Liga na mpaka sasa hawajapata point yoyote katika michezo minne waliyocheza.
Mwishoni mwa juma lililopita walipoteza kwa kufungwa mabao mawili kwa moja dhidi ya Athletic Bilbao, hatua ambayo iliongeza chachu kwa viongozi kuafiki maamuzi ya kumtimua meneja huyo kutoka nchini Hispania. Ayesteran anakua meneja wanane kutimuliwa na uongozi wa klabu hiyo, tangu mwaka 2012.
Kufuatia maamuzi hayo, kocha wa kikosi cha wakubwa klabuni hapo Salvador Gonzalez (Voro) ameteuliwa kuwa meneja wa muda, hadi hapo uongozi wa Valancia CF utakapompata mkuu wa benchi la ufundi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |