Mchezo huo ulimalizika kwa KRC Genk kuibuka na ushindi mnono wa magoli 3-1, magoli ambayo yalifungwa na Nikolaos Karelis dakika ya 8, mjamaica Leon Bailey dakika ya 25 na Thomas Buffel dakika ya 61 wakati goli la Sassuolo lilifungwa na Matteo Politano dakika ya 65.
Mtanzania Mbwana Samatta ambaye alikuwa majeruhi aliingia dakika ya 75 kuchukua nafasi ya mgiriki Nikolaos Karelis , ushindi huo wa KRC Genk unakuja ikiwa ni baada ya kukubali kipigo cha magoli 3-2 katika mchezo wa kwanza ugenini dhidi ya Rapid Wien, Genk sasa watacheza mchezo wao wa tatu October 20 dhidi ya Athletic Bilbao ya Hispania.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |