Katibu mkuu wa Shirika la kupambana na biashara ya wanyama na viumbe walio kwenye hatari ya kutoweka Bw John Scanlon, amesema wiki ya kwanza ya mkutano wa shirika hilo unaofanyika mjini Johannesburg imefanyika kwa mafanikio.
Katika wiki ya kwanza mkutano umepitisha mapendekezo ya Mexico, China na Marekani ya kuwaorodhesha samaki aina za Totoaba na Vaquita kama viumbe walio kwenye hatari ya kutoweka, na kwa mara ya kwanza umepitisha azimio kuhusu kupambana na ufisadi kwenye eneo hilo.
Umoja wa Ulaya na Senegal zimetoa pendekezo kuzitaka serikali kuchukua hatua za kupambana na ufisadi kwenye kupambana na vitendo vya usafirishaji wa wanyamapori.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |