Akizungumzia matunda ya udhamini wao Mkurugenzi wa Masoko wa TBL Group, Kushilla Thomas. alisema mwaka huu wameshuhudia mshiriki wa Kili Marathon akishiriki katika michezo ya Olimpiki ya Brazil na kumaliza katika nafasi ya tano katika mbio za kilomita 42.
Kwa upande wake, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Pamela Kikuli ametaja zawadi kwa mbio za km 42 Kilimanjaro Premium Lager Marathon ni pamoja na – jumla ya Tsh milioni 20 kwa washindani wanaume na wanawake watakaoshika nafasi 10 za juu. Mshindi wa kwanza kutoka kila kundi atapata Tsh milioni 4 kila mmoja.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |