Mwanariadha wa Kenya, Daniel Wanjiru, ameshinda kwa kuandika muda bora kwenye mashindano ya arobaini ya TCS ya Marathon ya Amsterdam nchini Uholanzi. Katika mashindano hayo, Wanjiru alitumia muda wa saa 2:05.21 na kuipiku rekodi ya mshindi mara tatu, wa Marathon ya Amsterdam Wilson Chebet ya saa 2:05.36 mwaka 2013.
Wanjiru alifuatiwa na Wakenya wenzake, Sammy Kitwara, aliyetumia saa 2:05.45, na Marius Kimutai, aliyetumia saa 2:05.47.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |