• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Jose Mourinho afedheheshwa na Chelsea kwa kushushiwa tetemeko la mabao 4-0

    (GMT+08:00) 2016-10-24 10:08:39

    Jose Mourinho alifedheheshwa aliporudi katika uwanja wa Stamford Bridge baada ya timu yake ya zamani kuicharaza Manchester United.

    The Blues, ambao walimfukuza kazi Jose Mourinho kwa mara ya pili mwaka uliopita waliongoza kwenye sekunde ya 30 ya mchezo kuanza baada ya Pedro kupata mwanya katika safu ya ulinzi ya Man United. Gary Cahill alifunga bao la pili katika kipindi cha pili baada ya United kuruhusu kona iliyopigwa na Eden Hazard kudunda katika eneo la hatari la man United. United hawakuonyesha ishara yoyote ya kukomboa mabao hayo, hivyo wakaongezwa bao la tatu na Eden hazard baada ya mchezaji huyo kupiga mkwaju wa umbalii wa hatua 15. N'golo Kante aliimwaga safu ya ulinzi ya United na kufunga bao la nne na la mwisho na kuipatia ushindi Chelsea huku ikipanda hadi nafasi ya nne.

    United watasalia katika nafasi ya 7 huku pengo kati yao na viongozi wa ligi likiongezeka na kufikia pointi tano. Wakati huohuo viongozi wa Ligi Manchester City walitoka sare na Southampton katika uwanja wa Etihad.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako