Bingwa wa mwaka jana Rotich alitwaa taji lake kwa kutumia saa 2:10.
Rotich, 28, ambaye alishinda taji la Marathon ya Geneva nchini Uswizi mnamo Mei 8 mwaka huu, aliongoza Wakenya Titus Masai na Francis Maina Ngare kufagia nafasi tatu za kwanza.
Kwa upande wa Cherono, 36, na Mkenya mwenzake Ester Wanjiru Macharia walinyakua nafasi mbili za kwanza katika kitengo cha kinadada. Bingwa mara tatu wa marathon nchini Italia, Ivana Iozzia alikamata nafasi ya tatu. Cherono alikamilisha umbali wa kilomita 42 kwa saa 2:27, ni Mkenya wa kwanza kushinda mbio hizi tangu Mercy Kibarus mwaka 2013.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |