• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China haitairuhusu Marekani kuitumia vibaya Bahari ya Kusini ya China

    (GMT+08:00) 2016-10-24 18:37:11

    Gazeti la Chama cha Kikomunisti cha China People's Daily limeikosoa Marekani kwa kuruhusu meli yake ya kivita kuingia kwenye eneo la bahari la China katika Bahari ya Kusini ya China, na kusema vitendo kama hivyo vitaongeza kushuka kwa ushawishi wa Marekani.

    Makala iliyochapishwa kwenye gazeti hilo imesema, meli hiyo ya Marekani iliingia kwenye eneo la bahari la China karibu na visiwa vya Xisha ijumaa iliyopita.

    Makala hiyo imesema, hatua hiyo ya meli ya Marekani ni ukiukwaji mkubwa wa haki na mamlaka ya China na sheria za kimataifa, na kwamba hatua hiyo pia imevuruga amani, usalama, na utaratibu katika eneo hilo la bahari.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako