Wizara ya mambo ya nje ya China imefanya tafrija ya kuadhimisha miaka 45 tangu irudishiwe kiti chake halali kwenye Umoja wa Mataifa. Mjumbe wa taifa Bw. Yang Jiechi akihutubia maadhimisho hayo yaliyofanyika jijini Beijing amesema katika kipindi cha miaka 45, China imekuwa ni mjenzi wa amani na mchangiaji wa maendeleo ya dunia.
"China itaendelea kufuata njia ya kujiendeleza kwa amani, kushikilia sera ya kidiplomasia ya amani na kujiamulia mambo, na kujenga uhusiano wa kimataifa wa aina mpya unaozingatia ushirikiano na kunufaishana. China itaendelea kufuata njia za ushirikiano, maendeleo ya pamoja na pande nyingi kupitia kuimarisha ushirikiano wa kimataifa, na kuunga mkono uongozi wa Umoja wa Mataifa katika mambo ya kimataifa."
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |