Kampuni ya simu ya Huawei ya China imesaini makubaliano ya ushirikiano na kampuni za kuuza muziki za kimataifa na barani Afrika ili kuongeza kasi ya kuufanya muziki wa Afrika uwe wa kidijitali.
Katika mkutano wa kilele wa wadau wa Huawei kusini mwa Afrika uliofanyika mjini Johannesburg, Afrika Kusini, kampuni hiyo ilisaini mikataba na kampuni ya Spice Music, Mtech, CCA, na makampuni mengine ya muziki.
Mkutano huo uliohudhuriwa na washiriki zaidi ya 40 wa sekta ya muziki, ulikuwa na lengo la kuanzisha jukwaa la kukuza ushirikiano wa kidijitali barani Afrika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |