Meli hiyo ijulikanayo kama Ruian City kutoka Kundi la Meli la COSCO, ilipokea ujumbe wa kuomba usaidizi jana wakati ikiwa kwenye safari zake za kawaida kati ya Hawaii na Japan.
Kutokana na ombi hilo, maeneo mengine matano ya msako yameongezwa wakati meli hiyo tayari imeshatafuta kwenye maeneo kadhaa ambayo baharia huyo mwenye miaka 51 anaweza kuchukuliwa na maji. Guo anadhaniwa kuanguka kutoka kwenye chombo chake Oktoba 25, umbali wa kilomita 900 nje ya Hawaii na timu yake imesema inawezekana amevaa koti la kujiokolea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |