Rais Barack Obama wa Marekani ameonekana kumkosoa mkurugenzi wa idara ya upelelezi ya Marekan FBI Bw James Comey, kwa kutangaza maendeleo mapya ya uchunguzi kuhusu uwezekano kuwa mgombea urais Bibi Clinton alizembea na kuvunjisha siri za taifa kwa kutuma barua pepe za kiofisi kwa anuani ya binafsi, siku 11 kabla ya uchaguzi wa urais. Rais Obama hakumkosoa Bw. Comey moja kwa moja, lakini alionesha kutoridhishwa na hatua yake akisema si ya kawaida, na hatua hiyo hafikiwa baada ya uamuzi, na sio wakati taarifa hazijakamilika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |